<?xml version="1.0" encoding="utf-8"?>
            <rss version="2.0" xmlns:geo="http://www.w3.org/2003/01/geo/wgs84_pos#" xmlns:georss="http://www.georss.org/georss">
                <channel>
                    <title>TIGblogs - Miguel's TIGBlog</title> 
                    <link>http://kikenya.tigblog.org/</link> 
                    <description>What's on the minds of young leaders from around the globe?</description> 
                    <language>en-us</language> 
             
                <item> 
                    <title>MAPENZI</title> 
                    <link>http://kikenya.tigblog.org/post/355299</link> 
                    <description><![CDATA[Ni jambo lisilo eleweka kamwe. Je, mna habari kwamba hamna "UTUMWA WENYE MATESO MENGI KULIKO UTUMWA WA KIMAPENZI"? Mbona tusijihami dhidi ya misisimko? Kwa kuwa ni jambo la kuudhi sana mtu anapojihusisha na mapenzi ambayo kwayo hayana msingi dhabiti.<br />
Sijui iwapo nitakuwa kweli nikuwasilisha ujumbe kwa kuyanakili haya kuwa embe mbivu huliwa kwa uvumilivu?<br />
Pindi tu baada ya usuhuba kuonyesha ishara za kunawiri kama mumea uliotiwa samadi ndipo bahari ikaanza kuchafuka. Jameni mbona hili swala sio rahisi kulipuuza kama ilivyo kawaida kupuuza maswala mengine.<br />
Leugim ameelewa kuwa ya Mungu ni makuu na ya kuku ni Mayai.<br />
Uhusianao dhabiti kama alivyofahamu Leugim ulizolota kiasi cha haja.<br />
Binti aliyemdhani kuwa dhahabu kumbe kawa adhabu. Punde baada ya haya kutokea Leugim aogelea katika bahari ya luja(Depression), ninalodhihirisha wazi  kuwa aliyewachwa kaachiwa mengi. Leugim hana suluhu hata kukabiliana na pigo hili. Kwa sasa kwake Leugim amani imefunga milango na kutupa funguo kusiko fikika kamwe.<br />
Kuvunjika kwa usuhuba dhabiti ni maradhi kwa aliyeachwa.<br />
maumivu haya yabainisha upungufu wa taaluma ya utabibu, kwani hata matabitu hawana mbinu mwafaka ya kukabiliana nao.<br />
Nitaendelea..............................]]></description> 
					<pubDate>Wed, 09 Apr 2008 03:59:00 -0400</pubDate> 
					<guid isPermaLink="true">http://kikenya.tigblog.org/post/355299</guid>
					<georss:point>-1.3166667 36.8333333</georss:point><geo:Point><geo:lat>-1.3166667</geo:lat><geo:long>36.8333333</geo:long></geo:Point>
                </item>
</channel>
</rss>
